Saturday, August 25, 2012

Ni Mataji 44 kwa Walioondoka Arsenal 0 kwa Waliobaki

Imepita miaka saba sasa tokea Arsenal walipotwaa kombe lao la mwisho la maana, na tokea wakati huo wachezaji waliyoihama klabu hiyo kujiunga na klabu zingine wamekusanya jumla ya medali za ushindi 44! 
Na si haba Song na van Persie hawatosubiri muda mrefu kabla hawajajipatia vikombe kupitia timu zao mpya.
Hapa FullSoka inaangalia ni vikombe vingapi wachezaji walioikacha Arsenal wameweza kupata ikiwa waliobaki hawajaambulia kitu. 

Tokea kulitwa kombe la FA mwaka 2005, Arsenal hawajaweza tena kutwaa kombe lolote kubwa na wameuza wachezaji wa kiwango cha juu 17 walioshinda jumla ya medali 44 kupitia timu 11 tofauti.
Samir Nasri akiwa na kombe la Premier League aliloshinda msimu 2011/12 
Thiery Henry, Cecs Fabregas, Samir Nasri, RVP na Song kwa kuorodhesha wachache waliihama Arsenal kwenda kutafuta makombe kama tukiamini maneno yao.

Arsenal imejikusanyia jumla ya pauni milioni 163 kwa mauzo ya walioondoka, bila kujumuiasha pauni 39 milioni za mauzo ya RVP na Song. 
Tunaposema mataji makubwa tunaondoa Community Shield na vikombe vya namna hivyo kwenye ligi zingine.
Debayor: Kombe lake la kwanza kubwa alilipatia Real 

Unaweza sema mmmh, si wamekwenda timu kubwa, lakini wengine wamepata vikombe na timu ambazo hata kwa sasa hazipo tena kwenye ramani ya Ligi Kuu: PORTHSMOUTH (FA Cup- medali kwa Sol Campbell na Lassana Diara) na BIRMINGHAM (Carling Cup - medali kwa Seb Larsson na Alex Hleb).                                   


Mataji Waliyopata Wachezaji Walioihama Arsenal Tokea 2005

2005 ---  PATRICK VIEIRA akiwa Juventus: 3 Serie A titles (Inter), 1 FA Cup (ManCity).

2006 ---  SOL CAMPBELL akiwa Portsmouth: 1 FA Cup. 

2006 ---  ASHLEY COLE akiwa Chelsea: 1 Prem Lge, 4 FA Cups, 1 Lge Cup, 1 Champs Lge. 


2006 ---  SEBASTIAN LARSSON akiwa Birmingham: 1 Carling Cup.

2006 ---  LAUREN akiwa Portsmouth: 1 FA Cup. 

2006 ---  JOSE ANTONIO REYES akiwa R Madrid: 1 La Liga, 1 Portuguese Lge Cup 

                (akiwa Benfica), 2 Europa Lge, 1 Uefa SuperCup 

2007 ---  THIERRY HENRY akiwa Barcelona: 2 La Liga, 1 Spanish Cup, 1 Champs Lge, 

                1 Uefa SuperCup, 1 Club World Cup. 

2007 ---  LASSANA DIARRA akwa Portsmouth: 1 FA Cup, 1 Spanish Cup (akiwa R  

                Madrid), 1 La Liga.

2008 ---  MATHIEU FLAMINI akiwa Milan: 1 Serie A. 

2008 ---  ALEXANDER HLEB akiwa Barcelona: 1Champs Lge, 1 La Liga, 1 Spanish 

                Cup, 1 Lge Cup (akiwa Birmingham).

2008 ---  GILBERTO SILVA akiwaa Panathinaikos: 1 Greek Lge, 1 Greek Cup.

2009 ---  EMMANUEL ADEBAYOR akiwa Man City: Spanish Cup (mkopo R Madrid). 

2009 ---  KOLO TOURE akiwa Man City: 1 FA Cup, 1 Premier Lge.

2010 ---  FRAN MERIDA akiwa A Madrid: 1 Euro Super Cup.

2011 ---  CESC FABREGAS akiwa Barcelona: 1 Euro Super Cup, 1 Club World Cup, 1

                Spanish Cup. 

2011 ---  GAEL CLICHY akiwa Man City: 1 Premier League. 

2011 ---  SAMIR NASRI akiwa Man City: 1 Premier League.
.


WIKIENDI NJEMAAAAAAAAAAA!!!

Soma zaidi ...

Arsenal Kuuza Kiungo Mwingine AC Milan

Klabu ya Ac Milan kwa kinachoonekana mshangao kwa wengi wapo mbioni kumuhamisha kiungo mwingine wa Arsenal kujiunga na klabu hiyo ya San Siro, Sky Sports imedokeza.

Arsene Wenger Smile


Sky wanaendelea kudai kwamba kwa waonavyo wao Bosi wa Arsenal hatokuwa na pingamizi juu ya jambo hilo na ataruhusu kiungo huyo aondoke bila ugumu wowote.

Kocha wa Ac Milan Massimiliano Allegri yupo sokoni akitafuta kiungo mkabaji na Denilson ndiye hasa aliyeona anafaa.

Denilson kwa sasa yupo nchini kwao Brazil akiichezea klabu ya Sao Paulo kwa mkopo baada kushindwa kupata nafasi Arsenal.

Mbrazil huyo alianza kuchezea timu ya watoto ya Sao Paulo na kupanda ngazi zote za timu za vijana na mpaka kufikia kuwa nahodha wa timu yake ya Taifa Brazil(U-21) kabla Arsenal hawajamsajili August 2006.

Samba Boy: kuna uwezekano akaelekea San Siro 

Tofauti na alivyouzwa Alex Song na Robin van Persie kwenda Barca na United, ofa yoyote kuhusu Denilson itakuwa rahisi kwa Arsene Wenger kukubali kirahisi.

Kujua hasa kwa nini Ac Milan wamevutiwa naye ni vigumu kuelewa lakini labda Bosi huyo wa Rosseneri anajua nini anataka kutoka kwa kijana huyo wa miaka 24.

Kiungo Denilson alichukua muda kuzoea mfumo wa Arsenal ila alitokea kuwa mmoja kati ya wachezaji wa kikosi cha kwanza cha The Gunners mwaka 2008/09, akishiriki michezo 51. 

Baada ya hapo, kiwango duni alichokuwa akionesha katika miezi 18 iliyofuata ikawa sababu ya kupelekwa Brazil kwa mkopo.

Denilson: Alipojiunga na Sao Paulo kwa mkopo 

Na kuibuka kwa Jack Wilshare kulichangia kwa kiasi kikubwa kumuondoa na ikabidi atimkie Sao Paulo kwa mkopo kuokoa soka lake.

Wenger  amekua akijaribu kumuuza Denilson majira ya joto yaliyopita na iliposhindikana akamrudusha tena Sao Paulo kwa mkopo.

AC Milan inawezekana wanahisi kutokana na umri wa Denilson kuwa miaka 24 hivyo kuleta matumaini ya kufanya vizuri mbeleni. 

Kwa upande wa Arsenal ofa yoyote ya maana ni dhahiri itakubaliwa kwa kuwa si mchezaji anayeonekana kuwa kwenye mipango ya Arsene Wenger tena.

JUMAMOSI NJEEEEEEEEEEEEMA!!

Soma zaidi ...

Chelsea Wamnyakua Mnigeria Victor Moses


Chelsea wamekamilisha usajili uliokuwa na mizengwe wa Voctor Moses kutoka Wigan leo Ijumaa baada ya kufaulu uchunguzi wa afya na kukubaliana kuhusu mahitaji yake binafsi.
The Blues walishuhudia ofa zao nne zikikataliwa na Mwenyekiti wa Wigan Dave Whelan. Sakata hili lilidumu tokea msimu ulipomalizika.
Whelan aliwaudhi Chelsea kwa kuongea hadharani kuhusiana na ofa walizokuwa wakitoa kwa kile kilichotafsiriwa kama kutaka kupandisha bei iwapo timu nyingine ingejitokeza kumtaka. 
Roberto Di Matteo amefanikiwa kumpata Victor Moses baada ya ofa ya mara ya tano kukubaliwa na Wigan siku ya Alhamisi, na kuthibitisha kwamba wamekubali ofa mpya kutoka Chelsea.
Ada ya uhamisho wa Moses mwenye umri wa miaka 21 inaaminika kua takribani pauni milioni 9.

Moses: alionesha kiwango kizuri alipocheza dhidi ya Chelsea wikiendi iliyopita
"Timu ya Chelsea inafuraha kutangaza kumsajili Victor Moses kutoka timu ya Wigan Athletic," taarifa kutoka mtandao wa Chelsea umethibitisha.
Chelsea hawakusema urefu wa mkataba wa Moses, ambaye alijiunga na Wigan akitokea Crystal Palace mwaka 2010 na kiwango chake kikapanda hasa msimu uliopita.
Moses ambaye amefunga mara nane katika mechi 74 za ligi, alionesha kiwango kizuri katika mchezo wa hivi karibuni wa Ligi Kuu waliolala 2-0 dhidi ya Chelsea wikiendi iliyopita.


Ana kibarua kigumu cha kufikia kiwango cha juu Stamford Bridge
Ikiwa ni dhahiri anaonekana atakuja kuwa mchezaji hodari, Moses ana kibarua kizito cha kukuza kiwango chake kuzidi hata alichonacho sasa ili apate kudumu Stamford Brigde. 
Ugumu huo unakuja baada ya Chelsea kua na viungo wa pembeni wa viwango vya juu wanaocheza nafasi moja na Moses: wachezaji kama Eden Hazard,Juan Mata, Daniel Sturridge na Marko Marin.  
 Katika duru la kimataifa, Moses aliichezea Uingereza tokea akiwa shule mpaka kufikia kiwango cha timu ya taifa chini ya miaka 21 (U-21), ila aliamua kuichezea Nigeria baada ya Uingereza kusuasua kumuita katika timu ya taifa hilo ya wakubwa. 
Ameichezea Nigeria mechi yake ya kwanza mwezi Februari mwaka huu dhidi ya Rwanda. 
Moses ni mchezaji wa pili kusajiliwa na Roberto Di Matteo ndani ya masaa machache, baada ya kumnyakua beki wa kulia wa Uhispania Cesar Azpolicueta kwa kitita cha pauni milioni 7 akitokea Marseille ya Ufaransa.
NAKUTAKIA JUMAMOSI NJEMA!!!!!!!!
Soma zaidi ...

Friday, August 24, 2012

David Silva Agoma Kurefusha Mkataba Mpaka Alipwe Sawa na Y. Toure


David Silva anaendelea kugomea kusaini urefushwaji wa mkataba wake na Manchester City mpaka ombi lake la kupewa pauni 200,000 kwa wiki sawa na Yaya Toure pamoja na Vicent Company likubaliwe.

David Silva happy to let Manchester City sweat in his quest to gain parity with club's £200,000-a-week top earners


City na Wawakilishi wa Silva bado hawajafikia makubaliano kuhusu mkataba huo mpya, ingawa mikutano baina ya pande hizo mbili yamekuwa yakifanyika tokea mwezi Juni.

Vizito wa City wanasisitiza hawana wasiwasi juu ya suala la Silva kurefusha mkataba na bado wana matumaini  ya kufikiwa makubaliano na Mspanishi huyo kurefusha muda wake wa kuwepo klabuni.

Ila, mapatano yanaonekana yataendelea ndani ya msimu huu kutokana na kushindwa kuafikiana na Silva mapema, tokea alipojiunga June 2010 akitokea Valencia amefanya vizuri sana hilo ndilo linalompa jeuri ya kuamua alipwe kiwango gani.

Akiongea baada ya ushiriki wake katika mashindano ya Ulaya 2012, Silva alisema: " Maajenti wangu wanakaribia kufikia makubaliano na City na inaonekana tutafunga dili muda mfupi kuanzia sasa."

The playmaker dazzled last season for Manchester City and helped Spain to the European Championship trophy this summer
Silva: anataka alipwa angalau sawa na Teves 

Alisaini mshahara wa pauni 130,000 kwa wiki alipojiunga akitokea Valencia, ila baada ya kuibuka na kuwa muhimu katika kikosi cha Mancini, Silva na wawakilishi wake wanaona kuna kila sababu ya kulipwa sawa na kina Yaya Toure na Vicent Kompany.

City walisitisha kupatana na mchezaji mwingine Nigel de Jong majira ya joto yaliyopita kutokana na kile walichokiona kuwa mapendekezo makubwa ya mshahara, ila kwa inavyoonekana mapatano na Silva hayatositishwa bali yataendelea kutokana na umuhimu wake kwenye timu.

Silva, ambaye alikiri kupata shida kuzoea mafundisho ya Mancini alipofika, yuko wazi juu ya kujifunga katika mkataba mrefu na City, ingawa vyanzo vya Uhispania vinadai Barcelona wanamuona kama ndiye mrithi wa mchezeshaji Xavi.

City wana sera ya kutokufanya mazungumzo ya mikataba na wachezaji katikati ya msimu.

Mkataba wa Silva utafikia kikomo Juni 2014, hivyo City bado wanamuda wa wa kutosha kuendelea na mazungumzo kwa kujidai mpaka wanakapofikia makubaliano.

 

Wachezaji wa City Wanaolipwa Zaidi

       - Yaya Toure: pauni 200,000 kwa wiki

       - Vicent Kompany: 200,000 kwa wiki

       - Carlos Tevez: 198,000 kwa wiki

       - Sergio Aguero: 190,000 kwa wiki

       - Emmanuel Adebayor: 175,000 kwa wiki (Ametimkia Spurs)

USIKU MWEMA!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!1
Soma zaidi ...

Nani Aondoa Ombi la Kuongezewa Mshahara Ili Abakie Man U


Nani ameondoa ombi lake la kutaka kuongezewa mshahara ili kuingia mkataba mpya Old Trafford. Mreno huyo na washauri wake wako tayari kukubali mshahara wa awali (basic Wage) uendelee kuwa ule ule anaopewa sasa ila awe bonus ndio ziongezwe.



Hali ya nani kuendelea kuwepo Old Trafford inatia mashaka. Ameondolewa kwenye kikosi cha mechi ya kesho dhidi ya Fulham baada ya mchezo usioridhisha Jumatatu dhidi ya  Everton katika uwanja wa Goodison Park. 


Ukichanganya na kiwango kibovu alichoonesha mwishoni mwa msimu uliomalizika, imekua ndio sababu ya msingi ya matakwa yake ya mkataba mpya kutupiliwa mbali na United.

Nani
Nani: Mambo magumu sasa ataka pungufu
Soma zaidi ...

Sahin Abadili Mawazo Sasa Aitaka Liverpool Badala Ya Arsenal


Hivi leo pametokea kutokuelewana kati ya Arsenal, Real Madrid na mwakilishi wa Sahin kuhusu makubaliano ya uhamisho wa kiungo huyo. 

Madrid wanataka wamtoe kwa mkopo kisha mwisho wa mkopo huo yafanyike mazungumzo juu ya kuchukuliwa jumla ama kuhitajika kurudi Bernabeu kitu ambacho hata Sahin ndicho anachoafiki, Arsenal wao hawataki habari za mkopo zaidi ya kutaka kumnunua jumla.

On the move: Nuri Sahin of Real Madrid

Nuri Sahin

Real walitoa saa 24 ili Arsenal kubadili msimamo wao, ila mpaka masaa hayo yanaishia upande wa kambi ya Arsenal ulikua kimya.

Mwakilishi wa Sahin alisafiri leo Alhamisi asubuhi kwenda Liverpool kukamilisha taratibu za Sahin kujiunga na timu hiyo, baada ya kuchoshwa na longolongo za Wapiga Bunduki Wa London. 

Kama FullSoka ilivyoripoti kwenye kurasa yake ya facebook (www.facebook.com/fullsoka) kukubali kwa Sahin kujiunga na Arsenal mwanzo wa wiki hii, baada ya kuwaambia Real kuwa Emirates ndio mahali alipochagua kwenda kwa mkopo.

Ila katika mazungumzo na mwakilishi wake Reza Fazeli, ilijitokeza kwamba Arsenal hawakutaka makubaliano ya mkopo badala yake kufanya manunuzi ya jumla kwa haraka.

Real hawakuwa radhi kwa hilo, kama ilivyokuwa kwa sahin, ambaye alikua anataka aende Arsenal kwa miezi 12 ili ajue kama Real watakua bado wanamuhitaji kabla hajaamua kujikita kwenye masuala ya kuihama jumla.

The Arsenal groundsman marks out the Emirates Stadium pitch

Emirates Stadium: hapa hasa ndipo Nuri Sahin anapotaka kuwepo kwa mkopo

Kwa upande wa Liverpool wanaafikiana na Real pamoja na matakwa ya Sahin, na ndio sababu jioni hii ajenti Fazeli yupo Merseyside kuweka wazi makubaliano na MD wa Liverpool Ian Ayre.

Mpaka sasa bado usajili haujakamilika na Arsenal wana nafasi bado, ingawa Real wanaamini kiungo huyo atakwenda Anfield, baada ya kuweka wazi wangependa aende huko.

Mapema leo, gazeti moja la Uhispania liliripoti kwamba hatma ya Sahin itajulikana ndani ya siku moja ijayo. 

Liverpool ndio ilikua timu ya kwanza kuonesha nia ya kumchukua, ila Sahin alipendelea zaidi kwenda Arsenal na alitaraji mpaka Jumanne iliyopita kua angekuwa ametimiza ndoto yake ya kucheza chini ya bosi wa Arsenal Arsene Wenger.

Gazeti la Macca waliandika kwamba Liverpool walitaraji kuwa wamekamilisha usajili huo wa mkopo kufikia leo Alhamisi jioni, ingawa gazeti la Mirror linaona suala bado ni tete kukamilishwa haraka kiasi hicho.

Gazeti lingine la Madrid liliandika kwamba Liverpool imejitokeza kua timu inayomfaa zaidi Sahin, kwani Sahin mwenyewe ana uhakika kwamba maneja wa Liverpool Brendan Rodgers atamuhakikishia nafasi kwenye kikosi kinachoanza kulinganishwa na Arsenal walio na viungo wengi.

USIKU MWEMA!!!!!!!!!!!!!!!
Soma zaidi ...

Thursday, August 23, 2012

Man U Kuuza Watatu Kabla Ya Dirisha la Usajili Kufungwa



Baada ya Mashetani Wekundu kufanya usajili unaoonekana kushiba, Sir Ferguson ana kazi pevu kuhakikisha baadhi ya wachezaji walio nje ya kikosi cha kwanza wanaotarajia kucheza kuwatoa kwa mkopo ama kuuza jumla.

Wachezaji kama Dimitar Berbatov, Federico Macheda na Bebe wanaonekana kutokua na nafasi hata la kukaa benchi hivyo wanaotakiwa kutafuta pori kuanzia sasa mpaka tarehe 31 (siku ya mwisho ya dirisha la usajili).

Pia imeripotiwa watu wa juu Old Trafford, wamesisitiza kua Nani na Hernandez hawataruhusiwa kuondoka Manchester.

Berbatov ana hamu ya kuondoka Man U, ila si kwa Bebe na Macheda ambao wangependa kubakia.

Dimitar Berbatov
Berbatov: Hana anachotamani zaidi ya kuondoka 
M-Bulgaria huyo ana uhakika wa kutakiwa na timu nyingi licha ya kua na umri wa miaka 31 baada ya kuchoshwa na benchi la Old Trafford.

Ferguson anaonekana kua mgumu kumuuza mchezaji huyo wa zamani wa Spurs kwa bei "chee" ila bado haijajulikana hasa Mzee huyo anataka kiasi gani.

Kuna hatari ya kuondoka bure msimu ujao iwapo hatoruhusiwa kusajili timu nyingine majira haya.

Ni vigumu kukisia timu gani zitahitaji huduma za Bebe na Macheda, kwa kuwa ni washambuliaji ambao kwa timu yoyote kuwachukua basi itakua ni kubahatisha.

Mreno Bebe ni maarufu sana! si kwa kucheza mpira bali kwa kununuliwa kwa kitita cha pauni milioni 7.4 bila hata Mzee Ferguson kuwa amemuona akicheza mpira.

Akiwa na miaka 22 sasa, msimu uliopita alikua kwa mkopo Besiktas ila maumivu ya kano (ligament) yalimfanya awe nje ya kiwanja kwa takribani miezi sita. Amerudi Premier League ila haonekani kuwa na future Old Trafford kwa kushindwa kwake kuthibitisha thamani yake.


Macheda: Nafasi ni finyu hata ya kukaa benchi  
Kwa upande wa Federico Macheda alionesha kua ni muona nyavu wa hali ya juu alipopewa nafasi kwa mara ya kwanza, akifunga goli muhimu na la ushindi dhidi ya Aston Villa muda wa majeruhi.
Hata hivyo Muitaliano huyo hajawahi fikia tena kiwango hicho na kupelekwa kwa mkopo Sampdoria na QPR havikusaidia kuchochea kurudi tena kwa kiwango chake.
Ferguson hatokuwa na nafasi ya wachezaji hao watatu msimu huu ukizingatia kuwepo kwa Wayne Rooney, Robin Van Persie, Chicharito na Danny Welbeck.
MCHANA MWEMA WA ALHAMIS!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Soma zaidi ...

Wednesday, August 22, 2012

Welbeck Akubali Kuongeza Mkataba Man United


Mchezaji chipukizi wa Uingereza Danny Welbeck mwishowe amekubali kuendelea kuwepo Old Trafford mpaka 2016 - amekuwepo hapo tokea akiwa na miaka 8.

Life's a bench: Danny Welbeck goes off, Robin van Persie comes on against Everton... still, he didn't do much

Welbeck amekubali kupigania namba yake licha ya kuwepo ushindani mkubwa                               

Mshambuliaji huyo wa Manchester United amesaini mkataba mpya wa miaka minne ambao utamfanya aendelee kuwepo klabuni hapo mpaka mwaka 2016.

Kwa mara ya kwanza mchezaji huyo alicheza mechi yake ya kwanza mwaka 2008 ila katika miezi 18 iliyopita amejikuta akiwa miongoni mwa wachezaji muhimu wa kikosi cha kwanza.

Alianza kucheza timu ya wakubwa mwezi March 2011 na kufanikiwa kuchaguliwa na timu yake ya Taifa kwenda kwenye mashindano ya Euro.

Ingawa United wamemsajili Robin kwa kitita cha pauni milioni 24 mapema mwezi huu hapakuwa na shaka Welbeck angekubali kusaini mkataba mpya.

One Lion: Welbeck's England career has taken off - here he is having a pop against Italy in the Polkraine

Welbeck akitupiamo dhidi ya Italyalipoiwakilisha Uingereza mashindano ya Euro 2012

"Danny amekuwa hapa tokea akiwa na miaka nane na amebadilika sana katika miaka ya hivi karibuni - kwanza akienda kwa mkopa na mwaka jana kama mchezaji wa kikosi cha kwanza," Sir Ferguson alinena kwenye mtandao wa manutd.com.

"Amekuwa mchezaji muhimu timu ya taifa pia, na kaonesha ukomavu wa utendaji wake Euro 2012.

"Mwaka huu utakuwa muhimu kwake, kuna matarajio makubwa juu yake."

Beck and haul: Danny Welbeck got among the goals for United last season, including here against Arsenal

Danny Welbeck hujituma na pia hufunga: hapa akiwa amefunga moja ya magoli dhidi ya Arsenal 

Welbeck, aliyezaliwa Longsight, alionesha furaha yake baada ya kusaini mkataba mpya na klabu yake tokea akiwa mvulana.

"Kuchchezea United ndio hasa nilichokua nataka kufanya - ni klabu niliyoisapoti maisha yangu yote," alisema.

"Nina hamu sana na msimu mpya ili nitoe mchango wangu kusaidia timu kushindania mataji.

"Nina jifunza kila mara kutoka kwa meneja bora na nina shauku hili liendelee nikiwa na wachezaji wakiwango cha dunia kikosini."

Welbeck amefunga jula ya magoli 17 ndani ya michezo 64 akiwa United tokea alipocheza mechi yake ya kwanza dhidi ya Midlesbrough katika kombe la ligi Septemba 2008.

PONGEZI KWA WELBECK KWA KUAFIKIANA NA MAN U, CHERIOOOO!!!!!!!!!!

Soma zaidi ...

Emmanuel Adebayor Auzwa Bei Ya Kutupa na Man City

                                                               
Sorted: The long-running Emmanuel Adebayor transfer story is done
Ade Mabao: Atalipwa mshahara wa pauni 175,000 kwa wiki. 

Emmanuel Adebayor amekamilisha mipango ya kuhamia Tottenham Hotspur kutoka Machester City kwa bei ya kutupa pauni milioni 5 tu.

Alifanya vizuri msimu uliopita , akichezea Tottenham kwa mkopo, alifunga jumla ya magoli 17 katika ligi kuu ya Premier.
Adebayor atakua mmoja kati ya wachezaji wa Spurs wanaolipwa mshahara mkubwa. 
Adebayor mwenye miaka 28, alikuwa akilipwa na Manchester City pauni 175,000 kwa wiki.
Mshambulizi huyo wa zamani wa Arsenal, alivujisha habari hizo kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter akiandika: Tottenham niko njiani! natamani magoli. Kaeeni tayari.
Mkataba wa Adebayor ulibakisha miaka miwili zaidi kama mchezaji wa Man City, ila tokea kuwe na kutokuelewana na Mancini amekua akipelekwa kwa mkopo kwenye timu kadhaa: (Real Madrid na Tottenham).
 " Nafurahi kujiunga moja kwa moja na Spurs baada ya klabu kuelewana na manchester City, alisema Adebayor.".
Tottenham na Man City hatimaye wafanya mapatano juu ya mshahara wa Adebayor wa pauni 175,000 kwa wiki 


"Pengine ilichukua muda mrefu kinyume na ilivyotarajiwa, lakini nimefurahi sana kurudi Tottenham Hotspurs. Nilifurahia sana nilipokua hapa msimu uliopita, na ni matumaini yangu tutaweza kwa pamoja kufanikiwa zaidi."
Inafahamika kwamba Spurs waligoma kumpa Adebayor mshahara wa pauni 175,000 kwa wiki.
Naye Adebayor aligoma akitaka apewe pauni 175,000 ama arudi City kukaa benchi kusubiria mkataba wake na City uishe huku akiendelea kulipwa kiwango hicho hicho. 
Mkataba wake kuisha maana yake atakua huru na pesa yote ya uhamisho atapokua anasajili timu nyingine itakuwa ya kwake.
Kwa kua Adebayor kurudi City atakuwa hatumiki huku akiendelea kulipwa pauni 175,000 kwa wiki kwa kipindi cha miaka miwili ijayo, City wakawa hawana jinsi ila wakubali kulipa zaidi ya nusu iliyobaki kujalizia mshahara kufikia pauni 175,000, na pesa hiyo ya kufidia ikitoka kwenye ada halisi ya uhamisho hivyo mwishowe City wakaambulia pauni milioni 5. 
Tottenham watamlipa pauni 80,000 kwa wiki, na Man City kufidia pauni 95,000 kwa kila wiki, ili kufanikisha makubaliano kati ya vilabu hivyo viwili.

JUMATANO NJEMA!!!!!!!!!!!!.
Soma zaidi ...