Saturday, August 18, 2012

Ferdinand apigwa faini kwa kumtukana Ashley Cole Choc

Rio Ferdinand apigwa faini kwa kumtusi Ashley Cole kwenye Twitter

Beki wa Manchester United Rio Ferdinand ametozwa faini ya pauni za Uingereza 45,000 sawa na dola za kimarekani $71,000 na chama cha mpira cha England baada ya kupatikana na hatia ya kutumia lugha mbovu kuhusu beki wa Chelsea Ashley Cole.
Kitengo huru imempata na hatia kwa kumkashifu Cole akitumia lugha inayopdhalilisha kwa msemo wa maneno 'Choc ice' kwa maana mtu mweusi nje na ndani mzungu.
Ferdinand alikanusha kua sivyo hivyo ila ni kwamba maanake ni mtu feki, au mnafiki.
Siku mdogo wa Rio Ferdinand: Anton Ferdinand walipokwaruzana na John Terry  
Matamshi yaliyopeperushwa kwa mtandao wa Twitter yalitokea baada ya Ashley Cole kutoa ushahidi mahakamani dhidi ya mdogo wake Rio aliyedai kua alitukanwa na John Terry. Terry hakupatikana na hatia.
Rio Ferdinand na Ashley Cole Twitter

Bosi wa United Sir Alex FErguson anaamini adhabu aliyopewa Ferdinand inaashishia hatari ya wachezaji mastaa kutumia Twitter. 
Ferguson alibainisha wachezaji wote wa United wamezuiwa kuongelea klabu on Twitter na amewaonya wale hujiachia kwenye mitandao kua wanatafuta matatizo na chama cha mpira FA.
"Ilikua dhahiri ingetokea. alisema baada ya faini ya Ferdinand. " Wanataka (The FA) kuvuia kabisa suala hili (Twitter)."
"Kinachonishangaza ni kwamba wachezaji wengine wamekua wakitweet kwa miaka sasa na hawajawahi kuulizwa chochote na FA.
"Sijui hasa inakuwaje mtu anajihusisha na Twitter. Ila ipo na kama klabu tumetoa maelekezo kwa wachezaji kwamba hawawezi kuiongelea klabu kwenye Tweeter
"Rio ni mtu mzima ila anatakiwa kujua neno moja tu linaweza tafsiriwa tofauti - na huwezi tena kulibadilisha."
England team-mates ... John Terry, Ashley Cole na Rio Ferdinand





No comments:

Post a Comment