Saturday, September 8, 2012

Kuondoka Ama Kubaki United, Mimi Sie Muamuzi - Wayne Rooney

Wayne Rooney amekubali kwamba mwenye maamuzi juu ya yeye kubakia United ama kuondoka si yeye.

Tokea kuwasili kwa mshambuliaji mwingine klabuni hapo Robin van Persie na Ferguson kua anamuanzisha benchi, ni dalili ya wazi hadhi yake klabuni hapo ipo hatarini.

Wayne Rooney
Mahusiano kati ya Fergie na Roo si mazuri

Kuwepo kwa Danny Welbeck, Javier Hernandez na straika mpya Angelo Henriquez, Ferguson hawezi tena kuletewa maringo na Rooney kwa kua ana wachezaji mbadala kwa nafasi ya ushambuliaji.

 Rooney alisema; ' Mara zote nimekua nikisema kama nitaendelea kuhitajika hapa basi nitaendelea kuwa mchezaji wa Manchester United.'


Akikumbushia uamuzi wake wa kusema hadharani kwamba anataka kuondoka, 
Rooney alisema 'Ni dhahiri miaka michache iliyopita kulikua na jambo, ila nilijishukia na haraka nilisema nilifanya makosa.

'Ikiwa watu wanataka niendelee kua mchezaji wa Manchester United, hilo ndilo nitakalo kua.'



Kuja kwa Robin kuna maanisha Wayne si tena mshambulizji namba moja


Ferguson hafurahishwi na Rooney kuonekana kunenepa na kua mzito mwanzoni mwa msimu huu, na mahusiano ya wawili hao bado si mazuri tokea malumbano ya mchezaji huyo kutaka kuondoka na tabia zake kwa ujumla.

Hayo yanaweza pelekea Rooney kuondoka United, hasa ukizingatia Sir Alex hamtegemei sana kwa sasa.

Tokea Rooney anajiunga na Man U mwaka 2004, amekua na namba ya kudumu katika kikosi cha Sir Alex, ila kwa sasa kama atabaki basi itabidi azoee kuanzia bechi mara zingine ama ajenge maelewana mazuri uwanjani na van Persie ili ajihakikishie nafasi.

 'Huwezi fikiria tu utacheza,' alisema Rooney. ' Ila mara zote nimekua nikijituma sana kuhakikisha Bosi anachezesha.

'Nimepata jeraha hili ila najituma sana gym kuhakikisha kwamba wakati nitakapoambiwa niko poa kurudi kiwanjani, narudi uwanjani na kufunga magoli.

'Ni jambo zuri kwa meneja, na sisi tunatakiwa kuhakikisha tuna muumiza kichwa.
'Napanga kurudi kwenye timu na kujaribu kutengeneza maelewano kiwanjani na Robin.

'Tokea nilipojiunga na United nimekua na maelewano mazuri na kina Ruud van Nistelrooy, Louis Saha, Carlos Tevez, Dimiter Berbatov, Javier Hernandez na Danny Welbeck.

'Kwa washambuliaji wa sasa inanibidi kuendana na hali. Kama nikicheza nyuma yao ama kama mshambuliaji wa mwisho. Mara zote hua naweza na kufiti vizuri.' Rooney alitanabaisha.


Wayne Rooney of Everton celebrates scoring the equalising goal during the FA Barclaycard Premiership match between Arsenal and Everton
Enzi hizo: Roo anakubali mambo yamekua ni kupanda na kushuka tokea alivyoanzia Everton
JUMAMOSI NJEMA KWA WANA PREMIER LEAGUE WOOOOOOOTE!!!!!
Soma zaidi ...

Friday, September 7, 2012

Siwezi Hamia Man City - C. Ronaldo

Cristiano Ronaldo ameapa hawezi kamwe kujiunga na manchester City ikiwa Sir Alex Ferguson bado ni Bosi wa manchester United.

Staa huyo aliyenunuliwa na Madrid kwa kitita cha pauni milioni 88, hana raha Bernabeu - na hilo linawatoa udenda Manchester City.

Chanzo cha habari karibu na Ronaldo (27) kilisema: ' Cristiano siku zote yupo karibu na Alex Ferguson na mara kwa mara huwa wanaongea, Cristiano hawezi kufanya kitu cha kumuumiza Ferguson kwa kujiunga na mahasimu wao.'

Kama baba na mwana: Kuna maelewana makubwa kati ya Ronaldo na Sir Alex 

Huvi karibuni Ronaldo alielezea jinsi Sir alex Ferguson alivyomuhimu kwake.
Alisema: 'Nilipojiunga na United nilikua na miaka 18 na Ferguson ni kama baba kwangu. Alinifundisha vitu vingi sana.

'Nimefanya nae kazi kwa miaka sita na ni mtu mzuri sana, kocha mzuri sana. Sir Alex na Mourinho ni ni makocha bora kabisa Duniani.'

Ila Ronaldo kwa sasa hana furaha Real Madrid na anataka mshahara wa pauni  520,000 kwa wiki.

AlhAmisi NjEmA!!!!!!!!!!! 
Soma zaidi ...

Sagna Achukizwa Na Arsenal Kuuza Mastaa

Arsenal wanaingia tena katika sakata jipya la wachezaji wao kuhoji jinsi timu hiyo inavyoendesha masuala ya kuuza wachezaji muhimu.

Safari hii ni Bacary Sagna, ambaye anaishutumu timu hiyo kwa kuwauza Robin vab Persie na Alex Songi huko yeye mwenyewe akishindwa kuthibitisha kama ataendelea kuwepo klabuni hapo. 

Sagna aliliambia gazeti la L'Equipe: 'Pindi wachezaji wenu wawili bora wanapoondoka, lazima utaanza jiuliza maswali.

'Kuna wakati mashabiki hunifuata na mtaani na kuniuliza, cha ajabu hata mimi mwenyewe sijui.
'Kila mtu alijua RVP angeondoka, lakini sio Song.
'Bado mdogo, ana miaka 24 na akiawa amebakiza miaka mitatu katika mkataba wake. Tumepoteza sana.
'Baada ya msimu huu kumalizika nitabakisha mwaka mmoja.'

Alex Song poses with former Spanish football player Andoni Zubizarreta (L) and Barcelona's deputy sporting director Josep Maria Bertomeu
Haijampendeza Sagna kuona Song anakwenda Barca
 Ingawa ametoa madai hayo, inasemekana Arsene Wenger leo kaamuru yaanze mazungumzo na wawakilishi wa mcheaji huyo juu ya ofa mpya ili akubali kuongezea mkataba na timu hiyo.


Sagna kwa sasa anapokea pauni 60.000-kwa-wiki ila anatarajia kupata nyongeza ya mshahara kama atakubali kusaini mkataba mpya.
Hali hii kama Samir anavyoonekana ndio anayoitaka Sagna, makombe!
Sagna- ambaye hajawahi kupata kombe lolote akiwa Arsenal - aliongeza: ' MImi ndiye mchezaji pekee kwenye kikosi cha kwanza ambaye nimebaki kutokea 2007. Mwezi May, nilikua nikiangalia kwenye tv Manchester City wakipita mitaani kuonesha taji la Premier League na nikawaona Samir na Gael (Clichy) wakiwa wamebeba kombe, nami nataka pia kubeba makombe. 

SIKU NJEMA!!!!!!!!!
Soma zaidi ...

Uroho Wa Mshahara Mkubwa Wazuia Nani Kuuzwa Leo

Louis Nani ameendelea kujiweka njia panda na asijue hatma yake, baada ya jana kushindwa kuafikiana na Zenit St. Petersburg juu ya kiwango cha mshahara anachotakiwa kulipwa, hivyo ataendela kuwepo Old Trafford msimu huu. 

Rusia usajili wao ulifungwa rasmi jana saa sita usiku kwa masaa ya Ulaya, hivyo kulikua bado na uwezekano wa Nani kuondoka Man U ingawa dirisha la Usajili lilikua limeshafungwa Uingereza na sehemu nyingi za Ulaya.


Nani ambaye alikua ameruhusiwa kuondoka Manchester United, hataondoka tena kwa sababu ya mshahara mkubwa aliokuwa anataka awe analipwa na klabu hiyo. 

Nani ambaye pia bado hajakubali mshahara mpya aliotengewa na Mashetani Wekundu kama ataamua kubaki, yuko njia panda  Old Trafford kwani si tu amegomewa kukubaliwa kua analipwa pauni 130,000 kwa wiki bali hata uhakika wa nafasi kiwanjani hana.

Nani na GF wake wakiwa katika hafla kuchangia Unicef iliyoandaliwa na United 

Valencia na Ashley Young wanapewa kipaumbele kwa nafasi ya wingi, na kuja kwa van Persie na mchawi Shinji Kagawa kutafanya nafasi yake kuwa finyu zaidi.

Watu wa karibu yake wanasema kwamba Nani anajiona hathaminiwi United kama wachezai wengine. 

Aliondolewa kikosini baada ya United kupata kipigo katika mechi ya ufunguzi dhidi ya Everton na tokea wakati huo hana uhakika wa namba.


New boy: Shinji Kagawa is getting more game-time than Nani
Kagawa anapata nafasi zaidi kulika Nani

Mechi ya Jumapili dhidi ya Southampton aliingia zikiwa zimebakia dakika 29 akipishwa na Kagawa katika ushindi wa 3-2 ni mechi yake ya pili msimu huu, ikiwa haanzi ama akianza lazima atolewe.

ALHAMISI NJEMA!!!!!!!!!!!!
Soma zaidi ...

Ashley Cole Kuondoka Chelsea Bure

Chelsea bado wana matumaini ya kuafikiana na beki wa pembeni wa timu hiyo Ashley Cole juu ya mkataba wake mpya.

Jana iliripitiwa kwamba Cole alikua tayari ameamua kuihama timu hiyo bure majira ya joto yajayo baada ya kutokuridhishwa na muda wa mkataba aliokuwa aongezewe na Chelsea.


Inadaiwa Chelsea walimpa ofa Ashley Cole(31) ya kuongeza mwaka mmoja katika mkataba wake wa sasa uliobakisha mwaka mmoja kumalizikia. 

Ikizingatiwa kwamba kama Cole akikataa kusaini mkataba mpya aliobakiza mwaka mmoja tu, basi majira kama haya ya dirisha la usajili mwakani atakua huru kuondoka bure. 
Ashley Cole
Cole akikwepa maswali ya waandishi wa habari jana
Mwezi uliopita A. Cole alipinga vikali habari zilizokua zimezagaa kwamba alikua nataka aongezewe mshahara kufikia pauni 200,000 kwa wiki.

Chelsea hawataki kumpoteza Cole, na hakuna ubishi kama ataamua kugoma kusaini basi kuna timu kubwa za Ulaya zitamgombea.

Amekua akihusishwa na kumfuata Mourihno Real Madrid, pia kuna timu nyingi watataka kumshawishi kwa kumtengea dau kubwa alitakalo.

SIKU NJEMA!!!!!!!!
Soma zaidi ...

Thursday, September 6, 2012

Kikosi Kizima Cha Manchester United 2012/ 2013



Manchester United – Kikosi cha Wachezaji 25





1
Wachezaji

De Abreu Oliveira, Anderson Luis
Waliokuzwa Uingereza


No
2
Dias Correia, Tiago Manuel
No
3
Buttner, Alexander
No
4
Carrick, Michael
Yes
5
Hernandez Balcazar, Javier
No
6
Cleverley, Thomas William
Yes
7
De Gea Quinta, David
No
8
Evans, Jonathan Grant
Yes
9
Evra, Patrice Latyr
No
10
Ferdinand, Rio Gavin
Yes
11
Fletcher, Darren Barr
Yes
12
Giggs, Ryan Joseph
Yes
13
Kagawa, Shinji
No
14
Lindegaard, Anders Rozenkrantz
No
15
Almedia Da Cunha, Luis Carlos
No
16
Pereira da Silva, Rafael
Yes
17
Rooney, Wayne Mark
Yes
18
Scholes, Paul
Yes
19
Smalling, Christopher
Yes
20
Valencia Mosquera, Luis Antonio
No
21
Van Persie, Robin
No
22
Vidic, Nemanja
No
23
Welbeck, Daniel
Yes
24
Young, Ashley Simon
Yes


Manchester United –  Chini ya Miaka 21 (Wanaweza Kutumika Bila Kuwemo Katika Kikosi Cha Wachezaji 25)


Barber, Benjamin Thomas
Barmby, Jack
Blackett, Tyler Nathan
Brady, Robert Brown, Reece Byrne, Sam John Cofie, John Erzuah Cole, Larnell James
Daehli, Mats Moeller
Dalley, Declan Michael Ekangamene, Charni Evans, Callum Leeroy Fletcher, Ashley Michael Fornasier, Michele Giverin, Luke
Gollini, Pierluigi
Gorre, Kenji Joel Goss, Sean Richard Grimshaw, Liam David Harrop, Josh
Hendrie, Luke John
Henriquez Iturra, Angelo Jose Hoelgebaum Pereira, Andreas Hugo Ioannou, Nicholas Dimitris
James, Reece
Januzaj, Adnan Johnstone, Samuel Luke Jones, Philip Anthony Keane, Michael Vincent Keane, William David
King, Joshua Christian Kojo Lawrence, Thomas Morris Lingard, Jesse Ellis
Love, Donald Alistair Macheda, Federico McConnell, Ryan Peter McCullough, Luke McGinty, Sean Andrew
McNair, Patrick James Coleman Pearson, Benjamin David Petrucci, Davide
Powell, Nicholas Edward
Rothwell, Joseph Matthew Rowley, Louis James Rudge, Jack James Sutherland, Jonathan David Thorpe, Thomas Joseph

              Tunnicliffe, Ryan
  Van Velzen, Gyliano     Vermijl, Marnick Danny   Veseli, Frederic
  Weir, James Michael
Wilkinson, Matthew Gary
Willock, Matthew Wilson, James Antony Wootton, Scott James

Soma zaidi ...