Sunday, August 12, 2012

Sir Ferguson Awalaumu Arsenal! Mmmh


Hii si haki! Sir Alex Ferguson awalaumu Arsenal kuhusu Van Persie

Inapendeza kumuona Sir Alex Ferguson anapodai Arsenal hawamtendei haki juu ya Van Persie.
Fergie haelewi kwa nini Arsenal wamekua hawamtendei haki ili aweze kumnyakua mshambuliaji wao hatari kwa paundi 15 million. “Tumejaribu sana ila hakuna mafanikio. ni vigumu kuelewa kwa nini wanakua wagumu na kuendesha mambo yao kwa njia hii,” alinena.
Ukiachilia kusema kwamba kama Arsene Wenger angejaribu kumsajili Wayne Rooney kwa pesa kiduchu si tu kwamba naye(Ferguson) asingewaelewa Arsenal bali asingetoa ushirikiano wa aina yoyote ile kufanikisha suala hilo.
Acha Rooney, Fergie pia ana hasira kwa kumkosa Lucas Moura amabye amechagua PSG na si Manchester United, na anataka kujua kwa nini soka limekua ovyo: “Sielwei na ni maajabu klabu inaweza lipa paundi milioni 35.5 kwa mtoto wa miaka 19,” alisema.
Kama kumbukumbu zangu ziko sahihi nakumbuka, mwaka 2004, Fergie alitoa paundi milioni 28 kwa ajili ya kumnyakua Wayne Rooney.
Ukitumia hesabu za uwiano wa Mabenk ya Uingereza (Infation Aspect), paundi milioni 24 alizotoa kwa Wayne Rooney kipindi hicho ni sawa na paundi milioni  36.3 kwa pesa za sasa. Rooney akiwa na miaka 18 kipindi hicho.
Fergie. Kwa kweli ni ajabu.

We waonaje juu ya hili, toa maoni yako hapo chini!!!!!!!!!!!

No comments:

Post a Comment