Friday, August 17, 2012

Arsenal kumpa Jezi namba 10 ya van Persie Wilshere

Podolski amemuachia kiungo wa mwuingereza aliyekua majeruhi kuchukua jezi namba 10 - na ana shauku ya kuivaa kabla ya Christmas!

Christmas presence: Showing up before Santa is now Wilshere's target
Kurudi uwanjani kabla ya Christmas ndio tageti ya Wilshere 

Jack Wilshere atapewa jezi namba 10 ya mshambuliaji anayeihama klabu hiyo Robin van Persie - kwa kuonesha imani nae na kumpa moyo zaidi apone haraka.
Bosi wa Arsenal Arsene Wenger amekubaliana na hilo, ni kitu kitachompa ahueni kubwa Wilshere akiwa anapigania kupona majeraha yake ambayo yamemfanya asiweze kugusa mpira tokea msimu uliopita.
Chipukizi huyo wa kiingereza Wilshere, miaka 20, anatarajia kurudi uwanjani kabla ya Christmas baada ya kua nje ya kiwanja kwa zaidi ya mwaka kwa majeraha ya goti na misulia.
Wenger anamtaka ndiye awe fundi katikati ya kiwanja na hivyo atapewa namba hiyo  ambayo inayohusishwa na mchezaji fundi uwanjani.
Namba10 hua ina umuhimu sana Arsenal baada ya mdachi Dennis Bergkamp kuivaa,watu wa Mahusiano (PR) pia wanataka kutumia mwanya huo kukuza brandi zaidi na kuuza jezi za Wilshare akiwa ni kipenzi cha mashabiki wa The Gunners. 
Mshambuliai mpya Lukas Podolski alicheleweshwa kupewa namba mpaka sasa dhumini likiwa ni kuona kama van Persie ataondoka ama atabaki, ingawa alitakiwa kupewa ikiwa van Persie ameondoka, baada ya kujua mapenzi ya mashabiki wa Arsenal na Wilshare imebidi ajiweke pembeni, zaidi akijikita kuwazoea wachazaji wenzake na sistimu ya uchezaji ya timu.

No comments:

Post a Comment