Friday, August 17, 2012

Karibu Manchester! Picha za RvP akiwasili United kukamilisha usajili leo asubuhi


"Ni jambo kubwa sana kua na mchezaji mwenye uwezo wa van Persie kujiunga na kikosi chetu," amesema Fergie 

Hope they have warm hands! Van Persie arrives at Bridgewater Hospital
Van Persie akiwasili katika hospitali ya Bridgewaterkuchukua vipimo vya afya

Sir Alex Ferguson amesema Manchester United sasa wana kikundi bora cha mastaika kama kile kilichowawezesha kuchukua vikpmbe vitatu mwaka 1999.
Robin van Persie anakamilisha taratibu za usajili wa paundi milioni 24 kutoka Arsenal kwenda Old Trafford leo Ijumaa, akisaini mkataba wa miaka minne kwa mshahara wa paundi elfu 200 kwa wiki, alfajiri hii amewasili katika hospitali ya Bridgewater jijini Manchester kwa ajili ya uchunguzi wa afya.
ROBIN VAN PERSIE ARRIVES IN MANCHESTER
Heading in: wawakilishi wa United wakihakikisha Van Persie ameingia kwenye gati la Bridgewater


Na Ferguson anaamini kwamba washambuliaji wake wanne Van Persie, Wayne Rooney, Danny Welbeck na Javier Hernandez wanaweza kufikia ama kupita kabisa mafanikio waliyopata mashujaa waliochukua vikombe vitatu msimu mmoja mwaka 1999.
“Rooney na Van Persie ni wachezaji bora sana na ni jambo zuri kua nao wote,” alisema Ferguson. “kumsajili Van Persie kutatuongezea nguvu zaidi kwenye mashambulizi.
“Tukirudi mwaka 1999 tulikua na Dwight Yorke, Andy Cole, Teddy Sheringham na Ole Gunnar Solskjaer – washambuliaji bora barani ulaya kwa wakati huo.
“Ndipo tunapoelekea kwa sasa tukiwa na Wayne, Robin, Chicharito na Danny. Ni fungu la wachezaji bora sana nachoombea kwa sasa ni nipatie kuchagua combination sahihi.
Ferguson, akiongea katika uzinduzi wa ushirikiano baina ya United na kampuni ya kamali za mtandaoni Bwin, aliongeza kwamba: “Van Persie bado hajasaini, ila tumeshakubaliana ada ya uhamisho.
“Sasa yupo njiani kutokea London na tutampima afya. Nataraji kila kitu kitaenda sawa kama tulivyopanga.
“Agent wake pia yupo katika maongezi na CEO David Gill. Pia naomba, kila kitu kitakua shwari kufikia jioni.
“Nina uhakika atakua tayari kucheza mechi ya jumatatu dhidi ya Everton.”
wayne rooney robin van persie
Watch out Everton: Wayne Rooney na Robin van Persie wataanza mechi na Everton

GETTY

Hata hivyo kuna uwekano mshambuliaji mmoja wa Manchester United anaweza kujiunga na Arsenal.Click hapa ujue ni mchezaji gani.


Mashetani Wekundu: Rio Ferdinand akiwaongoza Manchester United mazoezini leo asubuhi


 Toa maoni yako kama una cha kuchangia hapo chini........Aljumaa Kareem na Mwezi Mtukufu

No comments:

Post a Comment