Thursday, August 16, 2012

Breaking News: Robin van Persie atua Manchester United

Cheers to jeers: Robin van Persie atarajie kuzomewa na mashabiki wa Arsenal ila ni furaha kwa Manchester United 

Mshambuliaji wa Arsenal striker Robin van Persie mwishowe amepata ruksa ya kuungana na Wayne Rooney Old Trafford. 

Arsenal wamethibitisha kukubaliana ada ya uhamisho juu ya mchezaji huyo na mahasimu wao wakubwa Manchester United.

Mwanasoka huyo aliyefunga jumla ya magoli 30 season iliyopita atasafiri kwenda Manchester siku ya Alhamisi kwa ajili ya makubaliano binafsi na kukamilisha uchunguzi wa afya kabla ya kutia saini.

"Arsenal Football Club inathibitisha kwamba imekubali kumuhamisha Robin van Persie kwenda Manchester United," imeandika website ya Gunners.

Van Persie, ambaye alieleza wazi nia yake ya kuondoka Emirates Stadium, anajitayarisha kusaini mkataba wa miaka minne kuwepo Old Trafford kwa paundi milioni 24, hiii ni kutoka kwa bosi wa Arsenal  Arsene Wenger. 

Mdachi huyo inavyoonekana ndiye atakayeongoza ngome kali ya mashambulizi ya Mashetani Wekundu, ikizingatiwa Wayne Rooney alimaliza nyuma van Persie kwa ufungaji akitikisa nyavu mara 27 msimu uliopita. Mashetani Wekundu pia wana chipukizi Danny Welbeck na Javier 'Chicharito' Hernandez kama washambulizi.

Sir Alex Ferguson inaonekana emefanikiwa kumpata mchezaji aliyemtamani kwa kipindi kirefu kwa kuwapiku majirani zao na mahasimu wakubwa Manchester City na Juventus kupata saini ya van Persie, pia wameshawaweka kibindoni chipukizi kutoka Crewe Nick Powell na kiungo wa kijapani Shinji Kagawa.

No comments:

Post a Comment