Maicon amewasili rasmi leo katika kambi ya mazoezi na kulakiwa na Mario Balotelli - mchezaji mwenza wa zamani wakati wakiwa wote Inter Milan.
Kuwasili: Maicon akiwasili katika viwanja vikuu vya mazoezi HQ huku akikaribishwa na Brian Kidd
Kijana huyo mpya City baada ya kuangalia mazaingira, alishuka katika viwanja vya mazoezi ambapo wachezaji wa City walikua wakijitayarisha na mechi yao ya ligi dhidi ya Stoke City itakayopigwa siku ya Jumamosi na kukutana wachezaji wote wa City ila alionekana kumfurahia zaidi Balotelli.
Bosi wa City alimnyakua beki huyo wa kulia mbrazil kwa pauni milioni 3 siku ya mwisho ya dirisha la usajili.
Marafiki wa zamani! Maicon akisalimiana na Balotelli (kushoto) na akimsalimia Muamerika mwenzake Tevez (kulia)
Maicon huchukuliwa kama mmoja kati ya wachezaji bora kabisa duniani, ingawa alipelekwa puta na Gareth Bale wa Tottenham katika mechi ya Champions League misimu miwili iliyopita.
Mbrazil huyo alicheza chini ya Mancini wakiwa Inter, kabla ya mkataba wa kocha huyo kumalizika na kujiunga na Mabingwa hao wa sasa wa Uingereza.
Utalii: M-Brazili Maicon akioneshwa mazingira kwa mara ya kwanza
No comments:
Post a Comment