"Ni jambo kubwa sana kua na mchezaji mwenye uwezo wa van Persie kujiunga na kikosi chetu," amesema Fergie
Robin van Persie anakamilisha taratibu za usajili wa paundi milioni 24 kutoka Arsenal kwenda Old Trafford leo Ijumaa, akisaini mkataba wa miaka minne kwa mshahara wa paundi elfu 200 kwa wiki, alfajiri hii amewasili katika hospitali ya Bridgewater jijini Manchester kwa ajili ya uchunguzi wa afya.
Na Ferguson anaamini kwamba washambuliaji wake wanne Van Persie, Wayne Rooney, Danny Welbeck na Javier Hernandez wanaweza kufikia ama kupita kabisa mafanikio waliyopata mashujaa waliochukua vikombe vitatu msimu mmoja mwaka 1999.
“Rooney na Van Persie ni wachezaji bora sana na ni jambo zuri kua nao wote,” alisema Ferguson. “kumsajili Van Persie kutatuongezea nguvu zaidi kwenye mashambulizi.
“Tukirudi mwaka 1999 tulikua na Dwight Yorke, Andy Cole, Teddy Sheringham na Ole Gunnar Solskjaer – washambuliaji bora barani ulaya kwa wakati huo.
“Ndipo tunapoelekea kwa sasa tukiwa na Wayne, Robin, Chicharito na Danny. Ni fungu la wachezaji bora sana nachoombea kwa sasa ni nipatie kuchagua combination sahihi.
Ferguson, akiongea katika uzinduzi wa ushirikiano baina ya United na kampuni ya kamali za mtandaoni Bwin, aliongeza kwamba: “Van Persie bado hajasaini, ila tumeshakubaliana ada ya uhamisho.
“Sasa yupo njiani kutokea London na tutampima afya. Nataraji kila kitu kitaenda sawa kama tulivyopanga.
“Agent wake pia yupo katika maongezi na CEO David Gill. Pia naomba, kila kitu kitakua shwari kufikia jioni.
“Nina uhakika atakua tayari kucheza mechi ya jumatatu dhidi ya Everton.”
GETTY
Hata hivyo kuna uwekano mshambuliaji mmoja wa Manchester United anaweza kujiunga na Arsenal.Click hapa ujue ni mchezaji gani.
No comments:
Post a Comment