Sir Alex Ferguson na Robin van Persie |
Sir Alex Ferguson alithibitisha jana kwamba wamekubaliana na Arsenal uhamisho wa paundi milioni 24, kwa Mdachi huyo ambaye leo hii atakua anafanya uchunguzi wa afya ili kumalizia taratibu za usajili.
"Sasa yupo Manchester United, ni bahati mbaya kwetu. Uhamisho ulikamilika leo mchana," Wenger aliiambia televisheni ya Ufaransa TF1.
"Si jambo zuri kupoteza wachezaji wa kiwango kile ila alibakisha mwaka mmoja na akakataa kuongeza kwa hiyo hatukua na jinsi tena."
“read more”
New No 10? Lukas Podolski ndiye atakayechukua jezi namba kumi.
Wenger pia alisema kwamba pesa walizopata kutokana na mauzo ya van Persie hazitotumika hivi karibuni, kwa kua ameshawanunua wachezaji wapya majira haya ya joto.
"Tumesha sajili (Olivier) Giroud na (Lukas) Podolski ambao kimsingi tuliwanunua kuziba pengo la kuondoka kwa van Persie," alimalizia.
|
'We had no choice': Arsene Wenger was forced to sell Robin van Persie |
Baadhi ya Mashabiki wa Arsenal walionesha kukerwa kwao na kitendo cha RvP na kuchoma Jezi namba kumi aliyokua akitinga |
No comments:
Post a Comment